Ticker

6/recent/ticker-posts

CHUO CHA MAENDELEO YA MICHEZO MALYA CHATOA MAFUNZO YA UONGOZI NA UTAWALA KATIKA MICHEZO

Uongozi wa chuo cha Maendeleo Malya mkoani Mwanza umesema utaendelea kuaanda mafunzo ya Uongozi na utawala katika michezo kwa lengo la  kuwajengea uwezo viongozi wa klabu za michezo za Wizara na Taasisi za serikali zinazojihusisha na micheoz na kupata wataalamu wenye ueledi

 

Makamu mkuu wa Chuo cha Mandeleo ya michezo Malya  kilichopo wilaya ya Kwimba  mkoani Mwanza  Salumu Mtumbuka amesema mafunzo ya michezo katika uongozi na utawala ni nyenzo za kuwawezesha viongozi kutimiza majukumu yao bila kuvuka mipaka ya kiongozi


 Salum Mtumbuka - Makamu mkuu wa Chuo cha Mandeleo ya michezo Malya 

Makamu mwenyekiti wa Utamaduni  Sports Klabu  kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Ester Munyuku anaona mafunzo hayo ni sehemu ya kuimarisha uwezo wa viongozi kuongoza klabu zao.

               Ester Munyuku - M/Mkiti Utamaduni  Sports Klabu 

Naye Mratibu wa michezo wa chuo cha Ualimu Mpwapwa cha Dodoma John Kipalamoto  amesema wamekuwa mstari wa mbele katika kuibua vipaji vya vijana nan tayari wanao baadhi ya vijana ambao wamekwenda kufanya majaribio katka timu ya TMA inayshiriki ligi ya Championship.


John Kipalamoto - Mratibu wa michezo wa chuo cha Ualimu Mpwapwa

Kwa upande wake mjumbe  kutoka Mamlaka ya viwanja vya ndege Dar es Salaam Neema Makasi ambaye amewakilisha timu ya Uchukuzi Sports Club anasema mafunzo hayo yamemtoa nje ya boksi hivyo anaamini elimu hiyo itawasaidia zaidi katika kusimamia timu kwa kuzingatia sheria kanuni  na taratibu kwa kutambua michezo ni afya, ajira na huimarisha mahusiana.


                        Neema Makasi  -   Kiongozi wa Uchukuzi Spors Club

  Mafunzo hayo ya siku sita katika uongozi na utawala yameandaliwa na uongozi wa chuo cha Maendeleo ya michezo Malya na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa michezo wakiwemo viongozi wa klabu za michezo za Wizara na Taasisi za serikai zinazojihusisha na michezo.

Mwisho




Post a Comment

0 Comments