Wagombea ubunge Jimbo la Chato Kaskazini na Chato Kusini
KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 2025
CCM WILAYA YA CHATO IMETOA KATAZO LA MIKUTANO ISIYO
RASIMI KWA WAGOMBEA UBUNGE
Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chato Mkoa
wa Geita Kwa kushirikiana na Sekeretalieti ya CCM Wilaya imetoa Katazo la
Mikutano isiyo Rasmi.
Katika hatua nyingine
kamati hiyo imetoa maelekezo mbalimbali Kwa Wagombea Ubunge katika Majimbo
Mawili ya Chato Kasikazini na Chato Kusini wakitakiwa kutii kanuni za
Uchaguzi,kukemea Vikari Siasa za Kuchafuana Kwa lengo la Kujenga
Umoja,Ushirikiano Kwa maslahi mapana ya CCM.
Akifungua kikao cha maelekezo Kwa wagombea Ubunge katika Majimbo Mawili ya
Wilaya ya Chato, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chato Barnabas
Nyilembe amewapongeza wagombea Kwa kujitokeza Kwa wingi katika nafasi ya Ubunge.
Kwa upande wa jimbo la Chato Kasikazini wamejitokeza
waombaji nafasi ya Ubunge 15 wakati Jimbo la Chato Kusini wamejitokeza wagombea
18 na kusisitizwa kwa pamoja kuacha
Siasa chafu za kuchafuana Kwa sababu Chama cha Mapinduzi kimejipanga kushinda
Kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Aidha Nyilembe amekemea wagombea kutumia Vitendo vya rushwa kuwashawishi
wajumbe ili kuwapigia Kura baada ya kuchaguliwa kwa majina matatu yatakapo
pendekezwa hali hiyo haikubaliki Kwa sababu ni ukwiukwaji wa kanuni za Chama
cha Mapinduzi na kwamba watakapobaini kukiuka kanuni hizo watawajibishwa.
Amesema Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chato kimejipanga kuangalia mienendo ya
Wagombea Ubunge ili kupata wagombea wenye Sifa zinazostahili kuwatumikia
mwananchi pia kukiwakilisha Vema Chama hicho kwa kuonyesha tabia nzuri kwa
jamii yetu ili kujenga heshima ya Wilaya ya Chato hivyo wagombea wanatakiwa
kuwa waadilifu,uaminifu, wazalendo na mwenye maono mapana kwa manufaa ya Taifa.
Awali akisoma kanuni za Uchaguzi za Chama cha Mapinduzi kwa wagombea Ubunge,
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Chato Charles Mazuri ametoa Katazo la Mikutano
isipokuwa Rasmi kwa kuzingatia kanuni inayosema kwamba kuongoza kura siyo
kigezo cha kuteuliwa hivyo atakaye fanya Makosa Chama hakitamfumbia macho na
badala yake atawajibishwa.
Aidha amewataka kuacha tabia ya kujichukia Sheria mikononi endapo watabainika
Changamoto Kwa wagombea na badala yake wanatakiwa kutoa Taarifa kwenye Ofisi za
Chama ili taratibu za kuchukua hatua zifuatwe Kwa majibu wa kanuni zinavyo
elekeza kwamba wagombea wanatakiwa kushirikiana, kujenga Urafiki,kuheshimiana
na Kupendana, ili kuimarisha Umoja uliopo ndani ya CCM .
Mwaka 2015 katika kura za
maoni wagombea Ubunge ndani ya CCM walijitokeza 47, wakati Mwaka 2020 wagombea Ubunge walijitokeza 54 likiwa
Jimbo Moja na baada ya Jimbo la Chato kugawanywa kuwa majimbo mawili Mwaka huu
2025 na kupatikana Jimbo la Chato kasikazini lenye wagombea Ubunge 15 na Chato
Kusini lenye wagombea 18 hali inayotoa taswira mpya kwamba idadi ya watu kugombea
mwaka huu kupungua idadi ikilinganishwa
na Mwaka 2015 na Mwaka 2020.
Mwisho
**********

0 Comments