Ticker

6/recent/ticker-posts

JAJI MKUU WA TANZANIA AAGIZA UFANYIKE UTAFITI WA MASHAURI YA MAUAJI NA UBAKAJI

 

Jaji mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma amewaagiza majaji wafawidhi wa mahakama kuu kufanya utafiti  ili kubaini chanzo cha uwepo wa kesi nyingi za mauaji katika mkoa wa Mara na za ubakaji katika mkoa wa  Mwanza.

Jaji mkuu wa  Tanzania Profesa Ibrahim Juma ametoa maagizo hayo Jijini Mwanza wakati  akifungua kikao kazi ambacho kimewakutanisha majaji wafawidhi wa mahakama kuu ya Tanzania.

Aidha Jaji mkuu huyo amesema karne ya 21 ya Sayansi na Teknoljia  ni muhimu  ikawa ni chachu ya utoaji haki kwa wananchi wenye changamoto za kimahakama kwa kutumia mifumo ya TEHAMA.

 



 Profesa Ibrahim Juma - Jaji mkuu wa  Tanzania 

Awali Jaji kiongozi wamahakama kuu ya Tanzania Daktari Mustapha Mohamed Siyani akitoa taarifa ya utendaji kazi amesema majaji wafawidhi wameweza kupiga hatua katika utoaji huduma kwa wananchi ikiwemo kupunguza mashauri katika mahakama zao  licha ya uwepo wa changamoto mbalimbali.


Mh. Mustapha Mohamed Siyani – Jaji Kiongozi mahakama kuu ya Tanzania

Nao baadhi ya majaji wafawidhi wa mahakama kuu ambao wameshiriki kikao kazi hicho wamesema yapo maeneo yanayotakiwa kufanyiwa utafiti na  kuahidi  kuzingatia mfumo wa TEHANMA katika kutafuta ufumbuzi wa changamoto zilizopo. 


Mh.Dkt Ntemi Kilekamajenga – Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza
Mh.Rose Ibrahim – Jaji mfawidhi mahakama kuu kanda ya Morogoro

Kikao kazi hicho cha siku tatu kimewashirikisha majaji wafawidhi wa mahakama kuu ya Tanzania.

Mwisho

********

Post a Comment

0 Comments