Ticker

6/recent/ticker-posts

WATENDAJI WA KATA WASHAURIWA KUTOKIUKA SHERIA KANUNI NA TARATIBU ZA NCHI

 Sengerema

Mwanza

Watendaji wa kata nchini wameshauriwa kutokiuka  sheria kanuni na taratibu zilizopo na badala yake wanapaswa kuzizingatia wanapo wahudumia wananchi  katika maeneo yao.


 


 Mkufunzi wa elimu ya Uraia na Utawala Bora kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani Mrakibu masaidizi wa Polisi Iddah John ametoa Rai hiyo wakati  akitoa mada ya Ulinzi na Usalama wa Nchi katika mafunzo  kwa kamati ya ulinzi wilaya ya Sengerema, viongozi wa serikali za Mitaa katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na Buchosa mkoani Mwanza



                                                      ASP Iddah John – Mkufunzi wa mafunzo

Iddah amesema ni wajibu wa viongozi wote kufuata sheria kanuni, taratibu pamoja na miongozo iliyopo katika kuongoza.



                        Viongozi wa kamati ya Usalama

 Katibu Tawala wa wilaya ya Sengerema Cuthbert Midala akifungua mafunzo hayo amewasisitiza washiriki kuyatumia kwa malengo yaliyokusudiwa kwa kutambua elimu hiyo ni muhimu.


                                       Cuthbert Midala   Katibu Tawala wilaya ya Sengerema aliyesimama

 Dorice Dario ni Wakili wa serikali ambaye ni Mratibu wa mafunzo kutoka Wizara ya Katiba na Sheria ameyataja baadhi ya malengo kuwa ni Pamoja na kuwajengea uwezo viongozi wanaosimamia serikali za mitaa, wataalam katika Halmashauri na watendajki wa kata ili kuongoza kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pia  viongozi wa serikali za mitaa kujengewa uwezo kuhusu wajibu Demokrasia na Utawala Bora

 


Dorice Dario - Mratibu wa mafunzo Wizara ya Katiba na Sheria

 Kwa upande wake mtendaji wa kata ya Nyehunge Judith Mathias   Pamoja na Mtendaji wa kata ya Ibisebageni Masija Haruni ambao wameshiriki mafunzo hayo wameishukuru serikali na kusema yametolewa kwa muda mwafaka na kuahidi Kwenda kuyatumia kikamilifu.

  

                                                        Judith Mathias – Mtendaji kata ya Nyehunge



                                      Masija Hruni – Mtendaji wa kata ya Ibisebageni

Wawezeshaji wa mafunzo hayo wanatoka OR- TAMISEMI, Wizara ya Katiba na Sheria,Wizara ya Mambo ya Ndani kutoka Polisi,  Pamoja na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na mada mbalimbali zimetolewa ikiwemo Demokrasia na Utawala Bora, Ulinzi na Usalama wa nchi.

Mwisho

********

 

Post a Comment

0 Comments