Kukosekana kwa elimu ya kutosha na uhapa wa mashine za
kupimia afya ya udongo kumetajwa kuwa kikwazo cha wakulima wengi kushindwa
kulima kilimo cha tija Wilayani Magu mkoani Mwanza.
Hayo yamebainika katika ziara ya madiwani, wataalam wa kilimo wa halmashauri ya wilaya ya Magu mkoani Mwanza ambayo imeongozwa na kaimu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Marco Minzi diwani wa kata ya Bukandwe.
Mh. Marco Minzi – Diwani kata ya Bukandwe
Kwa upande wake Afisa kilimo wa wilaya ya Magu Baguna Linus amesema kuna uhaba wa mashine ya kupimia afya ya udongo katika mashamba ya wakulima lakini pamoja na changamoto zilizopo ipo mikakati ya kuwanusuru wakulima hao kwa kununua mashine zingine ili kila tarafa iwe na mashine ya kupimia afya ya udongo.
Baguna Linus – Afisa kilimo wa halmashauri ya wilaya ya Magu
Ziara hiyo ya kutembelea mashamba ya wakulima katika Kijiji cha Bundilya kata ya Kahangara ni sehemu ya kujifunza kwa madiwani hao ambao wameahidi kwenda kuwasisitiza wakulima kulima kilimo cha kisasa kwa kupima afya ya udongo na kuweka mbolea.ya samadi kwenye mashamba yao.
Mh.Faustine John – Diwani kata ya Kongolwa
Mh.Faustine Makioki – Diwani kata ya Sukuma
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya maendeleo ya Gavernance Links Daktari Donald Kasongi amesema ni muhimu afya ya udongo ikapimwa ili wakulima waweze kulima kilimo chenye tija kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi.
Dkt Donald Kasongi - Mkurugenzi wa Taasisi ya Maendeleo ya Gavernance Links
Bundala Ramadhan - Afisa kilimo kutoka Dacca programme TAHEA
Mmoja wa wakulima wa Kijiji cha Bundilya kata ya Kahangara Reuben Mpugeji amewashukuru madiwani hao hao pamoja na watalam kwa kufanya ziara katika kijiji hicho na kueleza jinsi alivyokwisha nufaika na zoezi la upimaji wa afya ya udongo ambapo kwa sasa anauwezo wakuvuna magunia kati ya 20 hadi 30 kwa hekari moja tofauti na ilivyokuwa hapo awali kuvuna maguni matano au sita.
Reuben Mpugeji - Mkulima wa Kijiji cha Bundilya
Mwisho
0 Comments