Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha
amemsimamisha kazi Meneja wa Wakala wa huduma ya ununuzi serikalini GPSA wa
Mkoa huo Mayala Ambuli pamoja na Watumishi Wawili wa Wakala wa Barabara Tanroads)
kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.
Paull Chacha - Mkuu wa mkoa wa Tabora
Chacha amechukua hatua hiyo baada ya
kupokea Malalamiko kutoka kwa Wateja wa GPSA Mkoani Tabora pamoja na
viongozi akiwemo yeye binafsi kuwa Muhanga wa Lugha ambazo hazina staha kutoka ndugu Mayala.
"Leo asubuhi nimefanya ziara ya
kushtukiza katika ofisi ya Wakala wa huduma ya ununuzi Serikalini GPSA Mkoa wa Tabora, nikiwa Katika ziara hiyo
na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora nimemsimamisha Kazi kupisha
Uchunguzi ndugu Mayala Ambuli ambaye alikuwa ni Meneja wa GPSA mkoa wa Tabora
kwa tuhuma za Kutumia Madaraka yake vibaya, kutoa Lugha zisizo na Staha kwa
Wateja wa GPSA na Viongozi wa Serikali na kuwa na Utovu wa nidhamu
Kazini"Alisema Chacha Wakati wa kikao hicho.
Pia, Mkuu wa Mkoa Tabora Paul Chacha
amefanya ziara ya Kushtukiza katika Ofisi ya Wakala wa Barabaraba Tanzania TANROADS na kufanya kikao kifupi na Watumishi wa Ofisi
hiyo na kumuagiza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tabora Mhandisi Rafael kuwatoa
watumishi wawili wa Mzani mdogo wa Tuli ili kupisha Uchunguzi wa tuhuma za
kupokea rushwa zinazowakabili.
Aidha Chacha amewaasa watumishi wote wa Mkoa wa
Tabora, kufanya kazi kwa kufuata sheria, kanuni , taratibu na misingi ya utumishi wa Umma na si vinginevyo.
"Amesisitiza kuwwa akiwa bado anahudumu kwa nafasi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora hatakubali mtu yeyote au watu wanafanya makosa hasa ya Matumizi mabaya ya madaraka
kwa manufaa yao binafsi, kwamba atakuwa Mkali muda wote kwa watumishi wa aina
hiyo" Alionya Chacha
Kwa upande mwingine Chacha amewashukuru wananchi wa Mkoa wa
Tabora kwa kuendelea kumpa ushirikiano ikiwemo kumpatia taarifa moja kwa moja
juu ya watumishi ambao wanatumia vibaya ofisi zao au maeneo yao ya kazi na lazima hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya watumishi wa aina hiyo.
Amewahakikishia na kuwaondoa hofu Wananchi kuwa watumishi wote wameletwa katika Tabora kwa ajili ya
kuwatumikia na sio kutumikia madaraka yao ikiwemo kuwaonea hivyo nilazima misingi ya Utumishi wa Umma izingatiwe ili kila mwananchi anufaike na matunda ya serikali yake kwa kupata haki na huduma anayostahili kutoka katika sekta mbalimbali.
Mwisho
*********
0 Comments