NMB YAFANYA MKUTANO MKUU WA MWAKA
Mwanza
Serikali imewataka
wataalam wa Taasisi za kifedha kujikita
katika kufanya utafiti utakaosaidia kutoa fursa ya uwekezaji kwa vijana wanaojihusisha na
ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika ziwa victoria ili waweze kukuza uchumi wao na taifa kwa
ujumla.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Said Mtanda wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa NMB ambao umefanyika jijini Mwanza unaoenga kufanya tathimini ya mwaka uliopita na kuweka mikakati ya mwaka unaofuata
Said Mtanda
- Mkuu wa mkoa wa Mwanza
Aidha Mtanda amesema Mwanza ni habu ya kiuchumi kwa kanda ya ziwa na nchi za maziwa makuu hivyo
ni muda mwafaka kufanya uwekezaji ukiwemo
uchumi wa buluu kwa ufugaji kwa njia ya vizimba katika ziwa
Victoria.
Said Mtanda - Mkuu wa mkoa wa Mwanza
Kwa upande wake Afisa mkuu wa sekta binafsi wa NMB Philbert Mponzi amesema serikali imeendelea kuweka mazingira rafiki hivyo dhamira yao ni kuoa huduma bora
zenye tija zinaendelea kutolewa kwa
Watanzania.
Philbert Mponzi - Afisa mkuu wa sekta binafsi wa
NMB
Meneja wa NMB kanda ya
ziwa Faraja Ng'ingo anaona kufanyika kwa mkutano huo ni sehemu ya mikakati inayofanywa na uongozi wa Benki hiyo maka makuu katika kuendelea kutao huduma za kifedha kwa wateja wao.
Faraja Ngingo - Meneja wa NMB kanda ya ziwa
Naye meneja wa tawi la benk House NMB kanda ya Dar es Salaam Frednand Mpono ameushukuru uongozi na wkueelezea manufaa ya mkutano huo.
Frednand Mpono - Meneja NMB tawi la Benki House Dar es Salaam
Mkutano huo ambao
hufanyika kila mwaka umeshirikisha
uongozi wa NMB makao makuu, mameneja wa kanda nane za benki hiyo matawi 241, wataalam pamoja na watumishi.
0 Comments